njia za kuhifadhi chakula

 NJIA BORA ZA UHIFADHIJI WA CHAKULA

Chakula kinaweza kuhifadhia au kutunzwa kwa matumizi ya baadae kwa kupitia njia mbalimbali, watu wa zamani hawakuwa na technologia kama tuliyonayo wakati wa sasa hivyo walikuwa wakitumia njia mbalimbali kuhifadhi chakula kwa ajili ya matumizi ya baadaye,njia za kuhifadhi chakula zimegawanyika katika makundi mawili ambayo ni njia za kisasa na za asili

NJIA ZA ASILI

Hizi ni njia ambazo hutumia , vitu vya asili katika kufanya chakula kisiweze kuharibika,njia hizi ni kama zifuatavyo

  CHUMVI NA SUKARI

Hapa ni pale ambapo chumvi, sukari au vinega huwekwa au kupakwa katika  vyakula vya nyama ambapo husababisha chakula hicho kukauka kabisa na hivyo bacteria hushindwa kukaa mahali hapo na kukishambulia chakula hicho, mfano wa vyakula hivyo ni kama samaki, nyama nakadhalika, lakini pia njia hii husaidia kuongeza ladha nzuri kwenye chakula

KUKAUSHA JUANI

Njia hii hutumika kutunzia vyakula kama mahindi, mchelo,ndizi,maharage ,samaki ,mihogo, mboga za majani n.k

Njia hii ya kukausha na jua ni njia bora ambapo chakula huachwa juani kwa mda mrefu mpaka pale kitakapokauka kabisa na maji yote kuondoka na kukiacha chakula hicho kuwa kikavu kabisa hii hufanya bacteria ambao huaribu chakula kushindwa kabisa kukaa kwenye chakula hicho, vyakula kama ndizi na mihogo hukatwa katika vipande vidogo vidogo ili kuviwezesha kukauka haraka

MOSHI

Moshi pia hutumika katika kukaushia chakula ambapo chakula huwekwa juu ya kichanja na kwa chini moto huweshwa lakini kinachotakiwa ni moshi tu na sio moto, moshi wezeza kukausha chakula hicho na kuondo kiwango cha maji kabisha na kusababisha bacteria kushindwa kuishi humo, vyakula kama nyama,samaki na mbagomboga vinaweza kukaushwa kwa njia hii

KUPIKA

Kupika kunahusisha kuchemsha,kukaanga n.k njia hii ya kukipika chakula husaidia kuuwa bacteria ambao huwepo ndani chakula hizo na kukiacha kikiwa salama , vyakula kama viazi, ndizi , mihongo, samaki, nyama n.k vinaweza kuchemshwa kwanza halafu ndio vikakaushwa

UCHACHUSHAJI

Lakini pia chakula kinaweza kuchachushwa kwa mfano vyakula vya kabohydreti kama sukari huweza kubadilishwa na kuwa alcohol au maziwa freshi kubadilishwa na kuwa mtindi,vyakula kama matango na maembe huweza kuchanganywa na chumvi, na baada ya mtu lactic acid huzalishwa kukifanya chakula kuwa na ladha nzuri na kukiwezesha kukaa mda mrefu

NJIA ZA KISASA

KUTUMIA FRIJI

Hii ni njia ya kutunza chakula katika joto la chini sana ya sentigredi kutunza chakula katika joto la chini sana ya sentigredi  4  ambapo hufanya shughuli za bacteria kupungua na hivyo chakula huweza kudumu kwa mda mrefu bila ya kuharibika

UGANDISHAJI

Hapa ni pale ambapo chakula huweza kugandishwa kabisa chini ya nyuzi joto  -10 ambapo huzuia kabisha shughuli za bacteria wanaoharibu chakula kufanyika, vyakula mfano samaki, nyama vinaweza kugandishwa kabisa kwenye freezer na kufanya chakula kudumu kwa muda mrefu.

KUCHEMSHA (PASTEURIZATION)

Hii ni njia ambayo ilipewa jina na LOUIS PASTEUR ambapo chakula huchemshwa katika nyuzi joto za juu sana illi kuuwa bacteria ambao huleta uharibifu wa chakula, lakini pia njia hii husaidia kuongeza ladha kwenye chakula, vyakula ambavyo vinaweza kuchemshwa ni kama maziwa pamoja na juice za matunda

UYEYUSHAJI AU ULAINISHAJI WA VYAKULA

Hii ni njia ambayo hutumika kufanya vyakula kuwa katika mfumo wa kimiminika kwa mfano matunda husagwa na kuwa juice na kisha kuchemshwa  na kuwekwa kwenye makopo ya kuhifadhiwa

KUTUMIA KEMIKALI

Pia chakula kinaweza kuhifadhiwa kwa kutumia kemikali mbalimbali kama sodiam benzoate, sodiam chloride na vinegar huwekwa kwenye chakula kwa ajili ya kuzuia bacteria kufanya shughuli zao, hivyo husaidia chakula kukaa mda mrefu bila kuharibika

KUTUMIA MIONZI

Chakula kinaweza kupitishwa kwenye mionzi ambayo husaidia kuuwa bacteria waliopo kwenye chakula hicho na kukiacha kikiwa salama, vyakula hivyo vikiwemo  vitunguu, viazi, maharage n.k

 SOMA ZAIDI KUHUSU

Mlo kamili

Tabia hatarishi

Boresha afya ya akili

Jinsi ya kupunguza uzito

 

 

Post a Comment

Previous Post Next Post