TABIA HATARISHI
Tabia hatarishi hizi ni
tabia ambazo huweza kuweka maisha ya mtu kwenye hatari ya kuathirika kiafya
lakini pia huweza kuathiri hali ya kimwili na kiakili ya mtu Fulani, wapo watu
mbalimbali ambao wameathirika na tabia ambazo sio nzuri na zimeendelea kuwatesa
katika maisha yao, hapa nitaelezea baadhi ya tabia ambazo ni hatarishi katika
jamii na katika maisha ya mtu binafsi
UVUTAJI WA
BANGI NA KUTUMIA MADAWA
Wapo vijana ambao
hujihusisha na tabia kama hizi ambazo ni mbaya za uvutaji wa bangi pamoja na
utumiaji wa madawa ya kulevya, ambayo huweza kuleta madhara ya kiafya, pamoja
na kusababisha mmong’onyoka wa maadili,
uvutaji wa bangi pia huweza kuleta madhara mengi kiakili kwa mfano mtu anaweza kurukwa na akili kwa
sababu ya kuvuta bangi kupita kiasi
Pia utumiaji wa madawa ya
kulevya husababisha upotevu wa nguvu kazi kwa vijana, vijana wanaotumia madawa
ya kulevya hawawezi tena kufanya kazi ngumu na hata hamu ya kula hupungua
kadiri siku zinavyozidi kwenda
UKAHABA
Ukahaba ni tabia ambayo
huweka maisha ya wahusika katika hatari za kuambukizwa magonjwa mbalimbali ya
zinaa na ukizingatia yapo baadhi ya magonjwa ambayo hayana tiba kwa mfano
ugonjwa wa UKIMWI n.k vijana wengi hujihusisha katika tabia hizi za ukahaba na
hivyo kupelekea kukatisha ndoto zao za kimaisha ikiwemo kupata elimu n.k
MAPENZI
YASIYO SALAMA
Kitendo cha kujihusisha
na mahusiano na mpenzi Zaidi ya mmoja ni hatarishi sana lakini pia kushiriki
katika kufanya mapenzi bila hata ya kutumia kinga huweza kuweka afya ya mtu
katika hatari ya kupata magonjwa ya zinaa kama UKIMWI, KISONONO na KASWENDE
UENDESHAJI
CHOMBO CHA MOTO VIBAYA
Kuendesha gari,pikipiki,
bajaji nk vibaya kunaweza kupelekea ajali kutokea na mwisho kusababisha
vifo,lakini pia hupaswi kuendesha gari au pikipiki ukiwa umelewa na umetumia
madawa yanayoweza kuleta kizunguzungu, unapoendesha gari unapaswa kuvaa mkanda
na kuchukua tahadhari zote zinazotakiwa
ULAJI
MMBAYA
Ulaji mmbaya unaweza
kuweka afya ya mwili katika hatari ya kupata matatizo ya kiafya kwa mfano mtoto
anapokula kupitiliza anaweza akapata kiribatumbo, mtu ni lazima ale mlo
uliokamili ambao unamchanganyiko wa vitamini, madini n.k
Lakini pia vyakula
vinavyoongeza nguvu kama mihogo,wali,ugali,kande n.k humsaidia mtu kupata nguvu
ya kufanya kazi ngumu
Mtu ni lazima kuepuka
vyakula vyenye sukari nyingi kama keki,chokoleti nk sukari inapokua nyingi katika mwili huweza
kubadilishwa na kuwa mafuta hivyo huifadhiwa ndani ya mwili kwa matumizi ya
baadae hii huweza kupelekea kuongezeka uzito au unene baada ya mda Fulani.
KUJIDHURU
Wapo baadhi ya watu ambao
wanapojisikia kuvunjika moyo au kuchanganyikiwa huamua kujidhuru aidha kwa
kujiua au kujikatakata na viwembe ambayo huleta madhara makubwa katika mwili wa
mhusika n ahata kifo
UUZAJI
MBAYA WA BIDHAA AU UTEKAJI
Zipo bidhaa ambazo
zinauzwa kimagendo lakini pia zipo bidhaa ambazo ni hatarishi na
hazijathibitishwa na mamlaka husika kuweza kutumika katika jamii Fulani bidhaa
za namna hii huweza kuleta madhara makubwa katika jamii na hata kusababisha
kifo kwa mhusika, uuzaji wa bidhaa hizi
ni tabia mojawapo ambayo ni hatarishi na inaweza kumsababishia mtu kifungo cha
mda mrefu gerezani lakini pia wapo watu wengi ambao wamepotea katika mazingira
ya kutatanisha hii inatokana na kutekwa nyara na pengine hata kunyofolewa viungo
vyao kwa ajili ya pesa kujihusisha na tabia au makundi ya watu wa namna hii
kunaweza kupelekea kifungo, kifo au hata kufanyiwa kitu kibaya endapo mtuhumiwa
akikamatwa
UCHEZAJI WA
KAMARI
Kamari pia ni mojawapo ya
tabia ambazo ni hatarishi sana, watu wanaocheza Kamari pia hujihusisha sana na
tabia za wizi, uporaji, ukabaji na hata kuteka nyara, ni vyema kuwa makini sana
na watu wenye tabia za namna hii lakini pia kusaidia kuwarekebisha kama
itawezekana
BIASHARA
HATARI ZA MITANDAONI
Mtu pia anaweza akawa anajihusisha
na tabia hatarishi za mitandaoni ikiwemo
kufanya udukuzi kwenye account za watu kwa ajili ya kuiba fedha au taarifa
Fulani, lakini pia biashara haramu za uuzaji wa silaha,madawa ya kulevya n.k zinaweza pia kufanyika online
WAZO LA
MWISHO
Ni vyema kuzitambua tabia
hatarishi na kujua namna ya kuziepuka, baadhi ya tabia huweza kuleta
maafa,vifo, kuibiwa n.k ,zipo tabia nyingine nyingi ikiwepo unywaji wa pombe,
ubakaji, utapeli n.k
SOMA ZAIDI KUHUSU

