kuwa imara kimwili na kiakili

                    JINSI YA KUWA IMARA KIMWILI NA KIAKILI

Msingi wa kuwa na furaha ni kuwa na afya njema ya akili pamoja na ya mwili,kujiweka imara kimwili na kiakili kuna faida nyingi sana ikiwemo kuimarisha kinga ya mwili, kukusaidia kupunguza uzito kama una uzito uliokithiri lakini huupa ubongo nguvu ya kufanya kazi zake kwa ufanishi,

Mtu anapokuwa imara kiakili na kimwili huweza kufanya maamuzi kwa ufanisi, lakini pia humpa mtu nguvu ya kufanya kazi zake kwa bidi, pamoja na hayo uwezo wa kuwa imara kimwili na kiakili unapaswa uzingatie mambo yafuatayo

KUFANYA MAZOEZI

Ni lazima ujiwekee ratiba ya kufanya mazoezi kila siku au angalau siku 3 ndani ya wiki moja, mazoezi husaidia kupunguza kiwango cha mafuta katika mwili na hivyo humwezesha mtu kupungua uzito na ndo maana kwa wale ambao uzito wao umezidi wanashauriwa kufanya mazoezi mara kwa mara,lakini pia mazoezi huimarisha kinga ya mwili na kufanya akili kuwa imara, mazoezi mazuri ni yale yanayohusiana na kuongeza msukumo wa damu katika mwili, kunyoosha viungo, kwa mfano mazoezi kama ya kukimbia, kuruka Kamba n.k

EPUKANA NA MSONGO WA MAWAZO

Katika shughuli mbalimbali tunazozifanya huwa tunakutana na changamoto mbalimbali ambazo zinaweza kutusababishia kuwa na msongo wa mawazo, kutokana na hali hiyo ni muhimu kujua namna utakavyoweze kukabiliana na msongo wa mawazo,msongo wa mawazo unaweza ukakusababishia kuwa na hofu, maumivu ya kichwa,kukosa uelekeo katika malengo yako, soma Zaidi namna ya kukabiliana na msongo wa mawazo hapa

KULA MLO KAMILI

Mlo kamili ni muhimu kwa afya yako hivyo ni muhimu mtu apate mlo kamili ambao utakuwa na virutubisho vya aina mbalimbali pamoja na madini, vyakula kama ugali,wali,viazi, mihogo, maharage,mboga za majani, matunda n.k hivi vyakula huweza kuimarisha kinga ya mwili na kumfanya mtu awe imara kimwili na kiakili lakini pia mtu huweza kuepukana na magonjwa mbalimbali ikiwemo presha, mshtuko wa moyo,uzito uliokithiri n.k

PATA USINGIZI WA KUTOSHA

Kukosa usingizi wa kutosha kunaweza kuathiri afya ya mwili pamoja na ya akili hivyo inashauriwa mtu aweze kulala angalau kwa masaa saba au nane hii huufanya mwili pamoja na akili kupumzika vya kutosha na hivyo mtu anapoamka huwa na nguvu za kufanya shughuli zake kwa ufanisi

JALI AFYA YAKO

Afya yako ni muhimu sana lazima uhakikishe unakuwa msafi kwa kuonga na kuvaa nguo zilizo safi, kula mlo kamili hakikisha unajipenda mwenyewe kabla ya kuwapenda watu wengine, mara tu unaposikia dalili za kuumwa basi fika kituo cha afya mara moja kwa ajili ya kufanya vipimo mbalimbali vya mwili, ni lazima kujali afya yako kwanza epuka tabia hatarishi ambazo zinahatarisha afya yako au maisha yako kwa mfano unywaji wa pombe, uvutaji wa sigara, utumiaji wa madawa ya kulevya, ukahaba na mengineyo mambo kama haya hatarishi haupaswi kujihusisha nayo. jifunze zaidi namna ya kuimarisha afya yako ya akili hapa

TUMIA MDA WAKO WA ZIADA VIZURI

Unaweza ukatumia muda wako wa ziada kufanya mambo ambayo yataweza kuburudisha akili na mwili wako kwa mfano kucheza mpira, kutazama sinema, kwenda kuwatembelea ndugu na marafiki n.k  lakini pia waweza kuutumia mda wako wa ziada kupumzika. Ni vyema kujitengenezea ratiba maalum ya vitu ambavyo utakuwa unavifanya katika siku yako lakini pia ni lazima kujua kwamba muda wako wa ziada utautumia kufanya kitu gani ambacho kitakuletea manufaa na kukufanya ujisikie vizuri kiakili na kimwili pia.

NENO LA MWISHO

Ni vyema kujali afya yako na kuhakikisha kwamba mwili wako unakuwa imara kwa kushiriki mazoezi mbalimbali lakini pia unapaswa kuzingatia mlo kamili na kuishughulisha akili yako kwa kufanya kazi mbalimbali, jipende kwanza mwenyewe na kuwa nadhifu ndipo hapo itakapokuwa rahisi kuwapenda watu wengine, kumbuka kwamba afya yako ya kiakili na kimwili inapokuwa imara ndivyo itakavyokuwa rahisi kuweka malengo yako na kuyafikia kwa haraka

SOMA ZAIDI KUHUSU

Mambo 10 kuyajua unapokua mtu mzima

Namna ya kujenga afya yako ya akili

Jifunze kuhusu ndoto

Jinsi ya kuondoa harufu mbaya kwenye chumba

Mbinu za kupunguza uzito

Jinsi ya kuwa tajiri

 

 

 

 

 

 

 

Post a Comment

Previous Post Next Post