mambo muhimu ya kujua unapokua mtu mzima

 MAMBO AMBAYO UNAPASWA KUYAJUA UNAPOKUWA MTU MZIMA

Wakati ulipokuwa mtoto ni tofauti sana na unapokuwa mtu mzima, zipo changamoto nyingi ambazo unapaswa ukabiliane nazo wewe kama mtu mzima, unahitaji kuwa na hekima ya kutosha ili uweze kuishi na watu waliokuzunguka vizuri hapa nitaelezea vizuri mambo ambayo wewe kama mtu mzima ni muhimu kuyajua na wakati mwingine hakuna mtu ambaye atakwambia haya mambo

1.YUPO MTU ANAEKUPENDA BILA KUJALI VILE ULIVYO

Katika maisha yako utagundua kwamba wapo baadhi ya watu wanakuchukia bila sababu za msingi au pengine wanaona wivu kutokana na mafanikio ambayo umeyapata lakini ukae ukijua kwamba yupo mtu ambaye siku zote atakupenda na atafurahia mafanikio yako

2. NDUGU ZAKO WANAWEZA WAKAWA MAADUI ZAKO WA KWANZA

Wewe kama mtu mzima lazima ujue kwamba sio kila ndugu yako anafurahia maendeleo yako na mafanikio unayoyapata wapo wanaojifanya wanakupenda na kukujali lakini ukionyesha dalili za kufanikiwa ghafla wanaanza kuchukia na kuona wivu hivyo huanza kupingana na jitihada zozote utakazokuwa unazifanya

3.KIPAJI CHAKO HAKITAONEKANA MPAKA UKIFANYIE KAZI KWA BIDII

Yawezekana wewe una kipaji Fulani lakini ukae ukijua kipaji chochote hakiwezi kuonekana mpaka ukifanyie kazi pamoja na mazoezi ya kutosha mpaka pale utakapokuwa umebobea ndipo hapo watu watakapoona kwamba waweza kufanya mambo yanayohusiana na kipaji chako kiurahisi nao watasema kwamba unakipaji au umepewa kipawa na mungu lakini ni lazima kwanza ukihangaikie

4.WATU HUWA NA TABIA YA KURUDIA MAKOSA YAO YALE YALE

Asilimia kubwa ya watu wameathirika na tabia Fulani ambazo sio nzuri na mara nyingi watu  hujikuta wakifanya makosa hayo hayo siku zote, hii ikiwemo matendo yasiyo mazuri na matukio, hii hutokana na kujizoeza vibaya katika maisha yao

5. JIPENDE MWENYEWE KWANZA

Kujipenda mwenyewe humuongezea mtu ujasiri lakini pia kujithamini, huwezi kusema kwamba unampenda mtu mwingine na wakati wewe mwenyewe haujijali, lazima ujipende mwenyewe kwanza ndipo utasema unawapenda watu wengine, vaa vizuri,kula vizuri, jithamini vile ulivyo, watu wengine wanapoona unajithamini ndipo hapo wataanza kuvutiwa na muonekano wako na kutamani kukufahamu kwa undani

6.KADIRI UNAVYOZIDI KUFANIKIWA NDIVYO UNAPASWA KUWA NA MTAZAMO CHANYA

Unapopandishwa cheo au kutoka levo moja ya maisha na kwenda nyingine ni muhimu kufahamu kwamba lazima uwe na mtazamo chanya kwa sababu sasa utakuwa unadili na watu wa aina mbalimbali ili uweze kufanya nao kazi vizuri hupaswi kuwa mtu wa kumuwazia mwingine vibaya kwa haraka, kama unatabia ya kuwaza mabaya juu ya watu wengine basi ukae ukijua mambo mengi unayoyafanya watu wengine wanaweza wasikusapoti kwa sababu watajua kwamba unawawazia mabaya hii hupelekea kuharibika kwa mahusiano aidha ya kikazi, kirafiki au kibiashara.

7. WATU WALIOFANIKIWA HUWA WAKATILI KATIKA UTENDAJI WA JAMBO

Hii ni kweli na nimuhimu ujue kwamba watu wengi waliofanikiwa huwa hawajali mawazo ya watu wengine au mtazamo wao, wao wanapoamua jambo basi jambo hilo ni lazima litekelezwe na ni lazima wafanye juu chini ili kwamba dhamira yao iweze kutimia, hivyo ni muhimu ujue kwamba kama wewe unahitaji kufanikwa katika mambo yako ni lazima kuwa na tabia hii ya kuwa na ukatili katika utendaji si kwa ubaya bali kwa ukali kuhakikisha kwamba jambo lako lazima lifanikiwe

8.LOLOTE UTAKOLOFANYA LAZIMA KUNA WATU WATAKUCHUKIA

Kaa ukijua kwamba huwezi kumfurahisha kila mtu, wapo watu ambao hata uwepo wako hawawezi kuufurahia jua kwamba kuna watu ambao huchukia hata kama ukifanya jambo zuri la kusaidia wengine au vyovyote vile utakavyofanya, hata sasa yupo mtu ambaye unaweza ukamjua au usimjua anakuchukia tu namna unavyoongea,kutembea au unapofanya kazi zako kwa hiyo ni muhimu kuwa makini sana hasa unapokuwa umetenda jambo zuri usije ukahisi kila mtu amekufurahia

9.MAJUKUMU HAYAEPUKIKI

Unapokua mtu mzima ni vyema kujua kwamba hutaweza kuepuka majukuma asilimia mia hata kama ukisema hutaoa au kuwa na watoto lakini bado utakuwa na majukumu katika familia yako kama kusaidia wadogo zako and ndugu zako, huwezi eti kwa sababu wewe umefanikiwa sana basi ukajitenga na ndugu zako kabisa hilo wala si jambo zuri mbele za watu na mbele za mungu

10. KAZI NDIO MSINGI WA MAFANIKIO

Hakuna njia nyingine ya kufanikwa kiuchumi na kimaendeleo kazi peke yake ndio jawabu la mafanikio ya mtu , mtu yeyote ambae ni mvivu wa kufanya kazi hawezi kamwe kuja kufanikiwa katika jambo lolote analotaka kulifanya, bidii ya kazi itakufanikisha na kukuridhisha moyo wako pale unapomaliza kazi yako , fanya kazi zako kwa bidii sana na kwa ustadi wa hali ya juu nawe utayafurahia maisha unayoishi

 SOMA ZAIDI KUHUSU

Kwanini maisha ni magumu

Jifunze kuhusu ndoto

Afya ya akili

Jinsi ya kufanikiwa kiuchumi

Tabia za mtu aliyefanikiwa

 

Post a Comment

Previous Post Next Post