JINSI YA KUJIEPUSHA NA MSONGO WA MAWAZO
Kupatwa na msongo wa
mawazo ni jambo ambalo kila mtu amelipitia au huwa linatokea mara kwa mara, kwa
sababu ya shughuli mbalimbali ambazo tunajihusisha nazo hutusababishia
mlundikano wa mawazo mbalimbali ndani ya vichwa vyetu, msongo wa mawazo huweza
kuleta madhara mbalimbali ikiwemo maumivu ya kichwa, mtu kukosa uelekeo wa
maamuzi lakini pia wapo watu ambao unaweza kuwaona hata barabarani wakiwa
wanaongea peke yao kitu ambacho kinaweza kuwa ni cha ajabu mbele ya macho ya
watu wengine, njia bora za kuthibiti msongo wa mawazo ni kama zifuatazo
KUFUNGA NA
KUOMBA
Ningesema kufunga peke
yako kusingekuwa na mantiki yoyote hivyo ni lazima kuomba pia, hii ni njia
nzuri sana ya kuepukana na msongo wa mawazo,unapofunga unapaswa usamehe
wengine,usiwe na hofu na kumwamini mungu, usikae na chuki au mawazo mabaya,
kufungu humpa mtu displini ya hali ya juu na hivyo huweza kujikontrol kuanzia
ufahamu wake na mwili wake kiujumla unaweza kufunga angalau siku mbili kwa wiki
hii itakuwezesha kukaa wiki nzima bila kupatwa na msongo wa mawazo,mfungo huuwa
nguvu ya maumivu ya moyo, chuki, huzuni, hofu n.k soma Zaidi mambo unayopaswa
kufanya unapokuwa kwenye mfungo hapa
EPUKA
KUTEMBEA UMBALI MREFU PEKE YAKO
Mtu anapokua anatembea
mwenyewe peke yake hii huupa ufahamu wake uhuru wa kutafakari mambo mbalimbali
kwa kina, mawazo huachiliwa kutoka kwenye ufahamu wako wa ndani(subconscious
mind) na kuja mfululizo kama maji yanayotiririka baada ya mda utajikuta huna
tena uwezo wa kukontrol mawazo yako, kama unatafuta wazo Fulani na ungependa
kutafakari sana basi mbinu hii ya kutembea umbali mrefu itakusaidia kupata
solution ya tatizo Fulani.
KUFANYA
MEDITATION
Meditation kwa maneno ya
Kiswahili ninaweza kusema ni kutulia sehemu na kutokuwaza au kufikiria jambo
lolote,kuweka mawazo yako kwenye eneo moja tu ndani ya dakika 20 au 30 na
kuendelea, mtu anapomaliza kufanya meditation hujisika vizuri na hupata tena
uwezo wa kukotrol mawazo yake hivyo meditation ni nzuri kwani humrudishia mtu
focas katika mambo ambayo anataka kuyafanya.
PATA
USINGIZI WA KUTOSHA
Kutokupata usingizi mzuri
kunachangia sana kumfanya mtu kuwa na msongo wa mawazo maana ubongo unakuwa
umechoka pamoja na mwili hivyo hutaweza kutenda jambo lolote kwa ufanisi au
ustadi, inashauriwa kwamba mtu anapaswa alale angalau masaa 7 au 8 kila siku,
unapopata usingizi wa kutosha unaruhusu mwili wako pamoja na ufahamu wako
kujitengenezea nguvu mpya ambayo itakusaidia kufanya shughuli zako pale
utakapoamka, wakati mwingine watu hawapati usingizi wa kutosha kutokana na
kusumbuliwa na madoto ya ajabu ajabu au ya kutisha hivyo ni muhimu kuwa na
hekima ya namna kuepuka ndoto mbaya, soma Zaidi kuhusiana na ndoto hapa
MAZOEZI
Kufanya mazoezi ni
mojawapo ya njia nzuri ambayo itakusaidia kuepukana na msongo wa mawazo badala
ya kukaa peke yako ukiwa idle unaweza kutumia mda wako wa jioni kwenda kufanya
mazoezi lakini pia mazoezi yanafaida nyinginezo nyingi ikiwemo kuimarisha kinga
ya mwili, kukupa afya njema ya akili na kukongezea focus katika malengo
yako ya kimaisha
EPUKA
KUTAFAKARI SANA
Yapo matatizo mengi
tunayoyapitia na tunahitaji kutafakari kwa mda ili tuweze kujua ni mbinu zipi
tutazitumia kukabiliana nayo lakini kutafakari kwa mda mrefu huweza kusababisha
hofu, mashaka hasa pale unapoona kwamba jambo lako halina ufumbuzi, hii
hupelekea msongo wa mawazo na mwisho mtu
huanza kujisikia vibaya,kukosa furaha na kupoteza focus katika maisha yake
hivyo tafakari kwa muda ukiona hakuna mafanikio endelea na shughuli nyingine
kwanza baadaye unaweza hata ukamshirikisha na mwenzako au kuomba ushauri juu ya
utatuzi wa jambo Fulani
JIWEKE HURU
Lazima uhakikishe
unalinda ufahamu wako kutokana na mtazamo hasi, epuka mawazo mabaya, mawazo
mabaya huweza kuumiza hisia zako kiurahisi na kukufanya kuwa mhanga wa mawazo
hayo, mawazo mabaya huchangia mtu kuwa na hofu,wasiwasi, mashaka na hata
kupelekea magonjwa mbalimbali ya moyo ikiwemo presha ya kupanda au kushuko,
mshuto wa moyo n.k
NENO LA
MWISHO
Jenga mfumo wa maisha
yako vizuri, kuwa na mahusiano na watu vizuri ambao wanaweza wakakushauri namna
ya kukabiliana na changamoto za kimaisha unazopitia, kula vizuri, upeka tabia
zisizo na manufaa, fanya kazi kwa bidii na siku zote onyesha uwezo na nia ya
kusaidia wengine hii itakusaidia pale siku na wewe utakapohitaji msaada watu wengine
nao watakusaidia kwa sababu ya tabia yako kuwa nzuri
SOMA ZAIDI KUHUSU
Mambo 10 kuyajua unapokuamtu mzima
Namna ya kujenga afyayako ya akili
Jinsi ya kuondoa harufu mbaya kwenye chumba

