JINSI YA KUBORESHA AFYA
YA AKILI
Afya ya akili ni nini?
Afya ya akili ni hali ya ustawi wa kifikra inayomwezesha mtu kukabiliana na mazingira yake, kuwa na hisia bora, akili isiyo na msongo wa mawazo, furaha, kutokuwa na wasiwasi na kadhalika hizi ni sababu zinazochangia afya njema ya akili, ingawa afya ya akili ni muhimu sio kila mtu ana afya njema ya akili baadhi ya watu wanapata ugumu na changamoto mbalimbali za maisha na hivyo kuathiri hali zao za kiakili lakini pia kutokana na aina mbalimbali za magonjwa ambayo mtu anaweza kuyapata au kuumia maishani hali ya afya ya akili inaweza kuathirika.
Lakini
hata hivyo kuna njia ya kuboresha hali ya afya ya akili katika maisha moja,
ikiwa mtu huyo atakuwa na bidii kufuata maagizo yote yaliyotolewa na mtoa
huduma wa afya ya akili au daktari.
Jinsi ya kuboresha afya ya akili?
Hapa
kuna baadhi ya mambo ambayo mtu anaweza kufanya ili kuboresha hali yake ya afya
ya akili
KULA MLO KAMILI
Mlo
kamili ni aina ya chakula chenye virutubisho vyote muhimu vinavyohitajika
mwilini, ulaji wa chakula chenye madini, vitamini, protini, wanga n.k ni muhimu
sana kwani vyakula hivi vinachangia sana afya ya mwili na akili pia,
virutubisho hivi vitaupa mwili nguvu na kumwezesha mtu kufanya shughuli zake
kwa ufanisi
Epuka
kutumia kafeini kupita kiasi, sukari, vyakula vya kukaanga, vyakula vyenye
viungo vingi na pombe kwa sababu ni hatari kwa mwili ambao kinga yake tayari ni
dhaifu.
Lishe
iliyokamilika husaidia kudumisha uzito bora wa mwili, lakini pia hupunguza
hatari ya kuambukizwa magonjwa ya muda mrefu kama saratani, kisukari, unene,
shinikizo la damu na magonjwa mengine yanayotishia maisha.
Baadhi
ya vyakula huimarisha hali ya kiakili na kuongeza afya ya akili kwa mfano kula
samaki kumeonekana kuongeza uwezo wa akili wa mtu(intelligent quotients).
FANYA MAZOEZI KILA SIKU
Kufanya
mazoezi ni muhimu sana, mazoezi yanaufanya mwili mzima kuwa na afya na
uchangamfu, inashauriwa mtu afanye mazoezi angalau dakika 20 hadi 30 kwa siku,
mazoezi yanaweza kusaidia kuboresha afya ya akili ya mtu.
Kuna
aina tofauti za mazoezi ambayo mtu anaweza kufanya kwa mfano mazoezi ya
anaerobic, yoga au kufanya shughuli za nguvu kama sehemu ya mazoezi lakini bora
zaidi ni kwamba mtu lazima afanye mazoezi ya kuchangamka(anaerobic) kama
kukimbia, kuruka, kucheza, kuendesha baiskeli na kadhalika,
Kwa
mfano, mtu anapokimbia huruhusu mzunguko wa damu katika mwili wake wote ikiwa
ni pamoja na kwenye ubongo wake, hii huongeza utendaji kazi wa ubongo kwani
damu inaweza kufika sehemu zote za ubongo.
JITHAMINI
Lazima
ujitendee mwenyewe na wengine kwa heshima, epuka kujichanganya na mambo yote
ambayo yatakufanya ujisikie vibaya, moja ya tabia kubwa ya watu waliofanikiwa
ni lazima ujifunze kujipenda, weka malengo yako juu na kuyafuata, hii
itakuongezea kujiamini,kujipenda,kuwa na bidi kwa ujumla huimarisha mfumo mzima
wa jinsi utavyofikiri na kuimarisha afya yako ya akili
KUNYWA MAJI MENGI
Inashauriwa
kuwa ni lazima mtu anywe maji mengi ili kuuwezesha mwili kufanya kazi vizuri,
maji yanauwezesha mwili kulainisha sumu kali mwilini kwa ajili ya kuzitoa nje,
hii huchangia katika kufanya afya yako ya akili kuwa nzuri na imara.
ONDOA MSONGO WA MAWAZO
Kwa
kawaida msongo wa mawazo huja na kuondoka jambo ambalo ni hatari ni kuruhusu
msongo wa mawazo uendelee kukutesa . Kuwa na mawazo na wasiwasi mwingi sio
nzuri kwa afya yako, kwa hivyo tumia mbinu za kupunguza msongo wa mawazo kama
meditation, jifunze ukimya unapokuwa peke yako ambapo unaruhusu akili yako na
mwili wako kupumzika kwa dakika chache bila kufikiria chochote, yoga na
kadhalika. Ili kuboresha hali yako ya kiakili ni lazima akili yako isiwe na
wasiwasi, woga, mawazo mengi jifunze kukuweka huru kiakili.
FANYA MAMBO YANAYOKUPA
FURAHA
Jitahidi
kufanya mambo ambayo yatakupa furaha katika maisha yako, fanya vitu ambavyo
unavipenda sana, hii itaondoa nafasi ya kupata msongo wa mawazo, hofu na
wasiwasi.
Wakati
fulani kufanya kile unachopenda hufanya akili yako kuwa huru, yenye afya na
inakupa furaha
ACHA TABIA YENYE
MADHARA
Tabia
mbaya kama kuvuta sigara, unywaji pombe sio nzuri kwa afya yako ya akili,
jifunze kujishughulisha na mambo mazuri ya kimaadili
Tabia
mbaya inaweza kuharibu sio tu hali yako ya kiakili lakini pia afya yako ya
mwili, unaweza ukajikuta unaanza kuugua kwa sababu tu za uvutaji wa sigara,
bangi au ukapata matatizo ya kiafya zaidi.
WEKA MALENGO HALISI
Epuka
kuchanganyikiwa na mambo yanayoweza kukupa matumaini ya uongo jifunze kujiwekea
malengo yenye uhalisia Malengo unayojiwekea lazima yawezekane na kufikiwa.
Fanya kazi ili kufikia malengo yako, soma vitabu zaidi, jifunze kutoka kwa
wengine, daima uchangamshe ubongo wako kwa maarifa zaidi. Acha uvivu na usiwe mlalamikaji
fanya bidii ili kuboresha kiwango chako cha maisha kwa ujumla
SOMA ZAIDI
Jifunze vyanzo vya ndoto mbaya
Jinsi ya kumjua nabii wa uongo
Mambo ya kufanya kwenye mfungo

