Mtu aliyefanikiwa

SIFA ZA MTU ALIYEFANIKIWA

Mtu yoyote ambaye amefanikiwa katika maisha yake huonesha sifa mbalimbali ambazo watu wengi ambao wamefanikiwa huwa nazo

 Hapa nitaelezea sifa za mtu ambae ana tabia za watu ambao wamefanikiwa katika maisha yao

MUONEKANEKANO WAKE

Mtu yoyote ambae amefanikiwa katika maisha yake ni lazima awe na muonekano mzuri na ninapozungumzia muonekano ninamaanisha ni namna anavyovaa, mtu aliyefanikiwa anavaa mavazi mazuri yanayovutia , mavazi mazuri huonesha kwamba mtu huyo anajijali na anajipenda

Lakini pia muonekana wa kimwili kama ni mwanaume lazima awe mwenye nguvu na imara,hivyo kama wewe ni mwanaume ni lazima ujenge tabia ya kufanya mazoezi,mwanaume yoyote lazima awe na muonekano wa mtu aliye imara

Lakini kama ni mwanamke lazima awe na uzuri unaovutia mwanamke ni lazima ajali muonekano wake, shepu yake, nywele zake,hivyo ni muhimu sana kwa mwanamke kujipenda na kujithamini

PESA

Mtu yoyote aliyefanikiwa ni lazima awe na pesa lakini si pesa tu ni lazima awe na mifumo thabiti ya kutengeneza pesa, hivyo mwanaume anapaswa afanye kazi kwa bidii ili aweze kutengeneza pesa za kutunza familia au kufanyia mambo yake,

Mwanaume ni lazima ujifunze kuwekeza pesa zake kwa ajili ya kutatua changamoto mbalimbali za kimaisha, na hata mwanamke lazima ajue ni namna gani anaweza kujipatia kipato kwa kufanya kazi kwa bidii kazi ambayo itampa heshima mbele za watu

Wapo watu mbalimbali hapa duniani ambao tunaweza kuwachukulia kama maroll model katika maisha yetu wamefanikiwa na wanajipenda lakini pia wanapenda kazi wanazozifanya

PENDA UNACHOKIFANYA

Ni lazima upende unachokifanya huwezi kufanikiwa kama hupendi unachokifanya, wakati mwingine pesa huwa hamna na kila kitu huonesha hali ya kukatisha tamaa, lakini kama unapenda unachokifanya huwezi kukiacha hata kama unapitia wakati mgumu

Uchunguzi unaonyesha watu ambao hufanya vitu kwa kulazimishwa mara tu wanapopata uhuru wa kuendelea kufanya au kuacha wengi huamua kuacha.

MARAFIKI ZAO NI WALE WALIOFANIKIWA

Ili uweze kufanikiwa ni lazima  uwe na marafiki waliofanikiwa, ukiwa na marafiki waliofanikiwa utaishia kupata pesa tu lakini pia utapata nafasi (opportunity) mbalimbali za kupata pesa ili kuendesha maisha yako

Kama marafiki waliokuzunguka hawajafanikwa basi utaishia kuwa kama wao , utafanya vitu wanavyofanya wao, utapiga story kama zao na wala hutajua namna pesa zinavyotengenezwa, kama wanavyosemaga vitu vinavyofanana hukaa pamoja.

KUWA NA MTAZAMO CHANYA

Asilimia kubwa ya watu waliofanikiwa wana mtazamo chanya, hupenda kuwachukulia watu katika njia nzuri ya kujaribu kuwaelewa changamoto zao na kujua namna bora ya kuishi nao, wapo watu ambao ni wakorofi,wenye hasira na hawakawii kuanzisha ugomvi hivyo lazima ujua namna nzuri ya kuishi na watu wa namna hiyo.

USIKATE TAMAA

Wapo baadhi ya watu ambao walijaribu kufanya vitu vikubwa na walikuwa na malengo makubwa lakini walipoona mambo yameanza kuwa magumu wengi waliamua kutafuta ishu zingine za kufanya, kukata tamaa ni adui mkubwa wa mafanikia kama unajisikia kukata tamaa tafuta namna utakavyojifariji ili mradi tu usiache jambo unalolifanya endapo kama una malengo makubwa kwa hapo baade

FANYA KAZI KWA BIDII

Bidii ya mtu huwa haipotei fanya kazi zako kwa ustadi wa hali ya juu hapa tunasema (be high performer), watu wanaofanya kazi kwa ustadi wa hali ya juu ni watu wanaofanya kazi sana na tunaposema kufanya kazi sana tunamaanisha fanya kazi kila siku katika masaa yaleyale ambayo umejipangia usiruke baadhi ya siku na kufanya kazi siku Fulani tu hii itakuchelewesha katika safari yako ya maendeleo,

KITABU CHA SHUGHULI ZA KUFANYA

Mtu yoyote ambae ana maono fulani ni lazima awe na kijitabu kidogo ambacho ataandika humo mambo muhimu ambayo anatarajia kuyafanya, kila siku uamkapo asubuhi hakikisha anaandika vitu vyote ambavyo unataka kuvifanya kwa siku hiyo pamoja na mda utakaozifanya shughuli hizo hii inaupa ubongo wako nafasi ya kujua ni mawazo ya aina gani yaje kichwani mwako katika siku hiyo, na wakati mwingine watu hujikuta tu wakifanya vile vitu ambavyo wameviandika kwanye note buk zao

JIFUNZE KUONGEA MBELE ZA WATU

Ndio! watu ambao wanauwezo wa kuongea na kutoa hoja huwa wanapata nafasi ya kupewa kipaumbele katika sehemu yoyote, jifunze namna kumshawishi mtu na kufanya mazungumza yenye maana mbele za watu, yapo makampuni mengi ambayo yanahitaji watu wanaojua namna ya kuongea na wateja na kupigia debe bidhaa Fulani, kutetea jambo Fulani kwenye taasisi au kundi la watu, mtu anapotoa hoja nzuri kwa ujasiri huyo huonekana ana ufahamu mwingi kupita wengine na ndiye mtu ambaye anaweza akapewa nafasi ya kufanya kazi Fulani kwa sababu ya uwezo wake wa kuongea

JIAMINI

Kujiamini ni muhimu mno, mtu ambaye hajiamini huwezi kupanga nae kufanya jambo lolote kubwa kila mtu mwenye uwezo mpana katika jambo lolote ni mtu anaejiamini na mara nyingi watu ambao wapo katika safari ya mafanikio hukutana na changamoto nyingi na nyingine huwa zina vitisho hivyo ni lazima ujiamini ya kwamba unaweza na hakuna jambo gumu ,kama wengine waliweza wewe una nini mpaka ushindwe?

 

Hebu jaribu kutafakari na kujiuliza hivi kwa mfano ungekuwa HUOGOPI CHOCHOTE HAPA DUNIANI JE UNGECHAGUA KUFANYA NINI? Fikiria kama ungekuwa huogopi kufa, wala jela, wala polisi, wala kiongozi, wala kazi , wala chochote kile, Je kwa kutumia ujuzi na hekima uliyonayo SI UNGESHAFANIKIWA SIKU NYINGI lakini kwa sababu ya uwoga watu wameamua bora wakae chini watulie na wasifanye chochote kitakacholeta tafrani.

 

KUWA MTENDAJI

Usipende kuwa mtu wa maneno matupu kama umepanga jambo basi anza kutenda moja kwa moja, wapo baadhi ya watu ambao wao kazi yao ni kupanga tu na kutafakari, atasoma vitabu vyote atasikiliza vitu vitakavyomtia moyo lakini hatochukua hatua yoyote, ni ajabu kuona watu wanalalamika kwamba mimi ni mnene, mimi sina shepu,mimi sina kazi, mimi niko hivi lakini mwisho wa siku hafanyi chochote amekaa tu kama mbulula anasubiri miujiza itoke mbinguni ije imfuate mtu wa namna hiyo hawezi kufanikiwa hata kidogo ataishia kuwa na matumaini kwamba siku moja na yeye atafanikiwa lakini ataona miaka inazidi kwenda tu .

NENO LA MWISHO

Mtu aliyefanikiwa na nguvu za kutenda kazi, hawezi kulalamika, huishi na watu vizuri, ana mtazamo chanya,huwa ni muongeaji mzuri katika kutetea maslahi Fulani,ni mtu mwenye maarifa,smart na anajitahidi kuonyesha matokeo mazuri katika kazi yake anayoifanya

Mtu yoyote aliefanikiwa ni mtu wa mfano wa kuigwa na mtu huyo anatafutwa na watu wengi ili awasaidie kuwaingizia pesa kwa sababu ya uwezo na ujasiri wake japo na yeye huwa na shughuli zake za kufanya.

Post a Comment

Previous Post Next Post