NDOTO MBAYA NI NINI?
NINI HUSABABISHA? NA JINSI YA GANI YA KUZIEPUKA?
Unapolala usiku unaweza kuona vitu ambavyo vinaweza kusumbua sana akili yako na moyo wako vitu hivi vinaweza vikawa vya kutisha, kuchukiza, kushtua na pia vinaweza kukatisha tamaa lakini aina hizi za ndoto huchochewa na kitu fulani katika maisha ya mtu, ndoto mbaya inaweza kumjia matu yeyote wakati akiwa amelala na wakati mwingine ndoto mbaya inaweza kutuonya juu ya jambo fulani ambalo linaweza likatokea katika siku za usoni.ndoto hudhihirika katika mifumo tofauti ya maono na wakati mwingine elimu ya kuhusu maono huitajika kuna miili tofauti inayotumika kwenye maono ya usiku bonyeza hapa kujifunza aina za miili
Hata hivyo, ndoto
hazitokei tu, ndoto husababishwa na mambo fulani ambayo tunayafanya katika
maisha yetu kwa mfano watu ambao tunakutana nao, mahali tunapokwenda, mambo
ambayo tunatazama, mambo ambayo tunafikiri na kadhalika.
Endapo kama hupendi
kabisa kuota ndoto yoyote mbaya wakati wa usiku na unataka kupata usingizi
mzuri sana, wa amani usiku basi kuna baadhi ya mambo mbalimbali ambayo wengi
hawayajui kuhusu ndoto, kwa sababu watu wengi hawana ujuzi wa ndoto, Hebu tuone
mambo ambayo yanaweza kusababisha ndoto mbaya
MATENDO/MATUKIO MABAYA
Ukishiriki tendo au
matukio mabaya unaweza ukaanza kuota ndoto mbaya matendo hayo mabaya
uliyoyafanya huweza kuja kama ndoto mbaya yakijielezea katika ndoto nini
maana ya ulichokifanya, uwakilishi wa ulichofanya/unachofanya au unatarajia
kukifanya utakuja kwenye ndoto zako hii inakupa fununu ya jinsi ukubwa wa madhara
ulivyo
Shughuli zote hizi
tunazozifanya aidha ni nzuri au mbaya tayari zimesemwa katika kanuni za MUNGU
na baadhi yake zinaweza kuelezewa na binadamu wa kawaida kulingana na mwenendo
wa maisha kwa mfano kuua kamwe si jambo zuri hauitaji kwenda shule kujua hilo.
KULALA NA NGUO/SHUKA CHAFU
Ninaposema najisi maana
yake ni kitu ambacho ni kichafu kiroho ukipatwa na ndoto mbaya jambo la kwanza
ningekushauri ufanye ni kuvua nguo ulizovaa na kubadilisha shuka baadhi ya nguo
tunazokuwa nazo tayari zimetumika katika shughuli mbaya. kabla hazijatufikia
hivyo unapolala roho yako inachanganyikana na nguvu zilizoko ndani ya nguo au
shuka ambayo unatumia hivyo utaweza kuona baadhi ya matukio yaliyowahi kufanywa
na mtumiaji wa nguo hiyo au shuka hiyo, nguo au shuka hutunza kumbukumbu za
matukio ya watumiaji wa vitu hivyo, maombi hayawezi kuondoa ndoto hizi mbaya bali
huondoa tu hofu ndani yako lakini ukirudia kulalia vitu hivyo utapata ndoto za
namna hiyo hiyo.
Kwa usingizi mzuri wa
usiku inashauriwa kununua nguo mpya ambayo haijawahi kutumika hapo awali au
kwenda kwa fundi cherehani na utengeneze nguo yako mwenyewe na shuka hii
itakuwezesha kuepuka kumbukumbu zote mbaya za matukio ambazo zimerekodiwa
katika nguo.
KULA CHAKULA CHA UCHAWI/MANUWIZO
Ikitokea umekula kitu chenye
uchawi hakuna unachoweza kufanya utaota ndoto mbaya usiku kucha hata ukiomba
haitafanya kazi maana chakula hicho kipo ndani yako, utakoota ndoto namna hiyo
mfululizo na unajua umekula sehemu Fulani ambayo una mashaka nayo basi kaa
macho usilale mpaka asubuhi mpaka pale ambapo chakula hicho kimeyeyuka na
kutoweka kabisa mwilini mwako.
Sehemu zingine ambazo tunaenda
kula sio za kuaminika, jitu linaweza kuweka kitu kwenye chakula kwa ajenda zake
zisizojulikana na inapotokea umekula hicho chakula basi ile nguvu mbaya
itajidhirisha kwako wakati wa usiku ambapo ndipo ambapo unaweza ukaona vitu vya
kishetaji ukiwa umelala hivyo hakikisha mahali unapoenda kula ni salama, safi
na pa kuaminika
KULALA BILA KUOMBA
Usipoomba halafu ukalala
ina maana kwamba huna ulinzi wa ziada, maombi kabla ya kulala ni muhimu sana
kwani unapoomba roho za kishetani haziwezi kukupata kwa sababu zinachukia
chochote kinachohusiana na maombi.
Ni vyema kusoma neno la
Mungu kabla ya kulala na kumkaribisha Mungu akulinde na mabaya yote yanayotokea
usiku. Unapoomba na kumkaribisha Mungu nafasi ya pepo wachafu kukupata ni ndogo
au sifuri hii itakupa usingizi mzuri wa usiku.
Na unapoomba funga ubavu
wa kushoto, kulia , juu na chini aina za ndoto pia husabishwa na ubavu
uliolalia kujifunza kuhusu ubavu nitaelezea kwenye Makala nyingine
KULALA BILA KUOGA
Kuoga ni muhimu sana
kabla ya kulala, hii ina maana kwamba unaondoa nguvu zote zilizokung'ang'ania,
ulipokuwa bize kazini ulikutana na watu wa aina mbalimbali na kuchangamana nao
baadhi ya watu hao hukuachia nguvu au nishati hasi wengine nishati chanya kwa
hivyo kuoga ni njia rahisi ya kuondoa nishati/nguvu yoyote iliyoambatanishwa na
wewe
Hapo zamani za kale
walitumia maji safi na chumvi kusafisha nguvu zote hasi zinazozunguka mwili na
kukuacha msafi, kulala na nguvu zisizo zako hupelekea kuota ndoto usiku usizozijua
na chanzo cha nishati kikiwa kibaya basi wewe utaota ndoto mbaya
KUANGALIA FILAMU FULANI
ZA KUTISHA
Kuangalia filamu zenye
matukio ya kutisha au matukio mabaya kunaweza kusababisha ndoto mbaya kwa
sababu kwa kawaida televisheni inaweza kuchangia ndoto zetu, hivyo ikiwa
unachotazama ni mambo ya kutisha basi kuna uwezekano mkubwa wa kupata ndoto za
kutisha ndoto hizi ni marudio ya mambo ambayo umekuwa ukiangalia.
Jinsi ya kuepuka ndoto mbaya
Kuoga kabla
ya kwenda kulala
Kuoga itakusaidia kukaa safi
na kuondoa nishati zote hasi zinazokuzunguka
Acha
kutazama filamu ya kutisha
Tazama tu sinema za
kawaida, filamu ya kutisha sio nzuri haswa kwa watoto, ikiwa hutaki kupata
ndoto mbaya wakati wa usiku basi acha kutazama sinema za kutisha.
Nunua nguo
mpya ya kulalia na shuka
Ni bora utafute nguo mpya
ya kulalia na shuka yake lakini hakikisha kitambaa ambacho hakijawahi kutumika
hapo awali, nguo yoyote iliyotumika itakuletea maono ya matukio aliyoyafanya
mtumiaji wa kwanza na wala hizo ndoto hazina uhusiano na wewe, ikiwa nguo ni
najisi basi utaota ndoto mbaya, kama sivyo basi pana tukio fulani ambalo
lilifanywa na mmiliki wa awali wa kitambaa hicho
Acha
kufanya maovu
Acha matendo yako maovu
yanadhuru wengine, ni bora zaidi wewe na kutenda mema kwa jamii kuliko
kuidhuru.
SOMA ZAIDI KUHUSU


