JINSI YA KUONDOA HARUFU
MBAYA KWENYE CHUMBA
Mara
nyingi sana kwenye vyumba tunavyoishi huwa kunakuwa na harufu mbalimbali ambazo
husababishwa na vitu tofauti tofauti kwa mfano mlundikano wa nguo chafu au nguo
mbichi , viatu ,soksi zilizovaliwa , au ukaribu wa chumba na choo au jalala au
uhifadhi wa vitu ambavyo havipaswi kuwepo ndani ya chumba,
Kuna baadhi ya vitu ambavyo hupaswa kuwekwa
stoo and sio chumbani hii hupelekea chumba kuwa na harufu ambayo sio nzuri,
zifuatazo ni njia ambazo unaweza kutumia kuondoa harufu mbaya kwenye chumba
Fanya usafi
Fanya
usafi na ondoa vitu vyote ambavyo havipaswi kuwepo chumbani ondoa manguo
machafu,viatu visafiswe,soksi zifuliwe,shuka za kulalia pia zifuliwe, futa
vumbi madirishani hapo utakuwa umekamilisha step ya kwanza ya kuondoa harufu
mbaya chumbani
Tumia air fresher
Air
fresher ni nzuri kwa ajili ya kupunguza au kuondoa harufu mbaya chumbani nenda SUPERMARKET
au kwenye maduka ambayo fresh air hupatikana, lakini sikushauri utumie perfume
kama air fresher kwa sababu perfume huwa na harufu kali kiasi ambacho huweza
kusababisha ukawa unapiga chafya tu
Tumia baking soda
Ndio
baking soda huwa ni nzuri katika kuondoa harufu kwa sababu baking soda hufyonza
harufu mbaya, hii hutumika pia kwenye kuondoa harufu mbaya za kwenye nguo kwa
kuilowekea nguo kwa mda Fulani, kwa hiyo chukua baking soda weka kwenye kikopo
au chupa kisha iache wazi basi yenyewe hufyonza harufu yoyote mbaya iliyopo
eneo hilo, tembelea duka lolote la
karibu huwa wanauza hizi baking soda
Tumia white vinegar
White
vinegar pia inasifika kwa kufyonza harufu mbaya iwe ni kwenye nguo au chumbani unaposafisha
au kudeki chumba unaweza ukaichanganya white vinegar na maji kisha ukayatumia
au simply iweke kwenye kopo na uiache wazi kazi yake itakuwa ni kufyonza harufu
mbaya kwenye chumba
Udi
Udi
unasifika sana kwa kuwa na harufu nzuri na ndio njia rahisi ya kuondoa harufu
mbaya kwenye chumba kwa haraka tembelea madukani ununue udi kisha uwe na tabia
ya kuchoma pale unapoona kuna harufu mbaya chumbani
Chemsha viungo na
matunda
Unaweza
pia ukakatakata malimao au machungwa ukatia kwenye sufuria ukaweka maji pamoja
na viungo kama iliki, abdalasini,karafu nk
Kisha
ukavichemsha vinapochemka hutoa harufu nzuri
baada ya hapo mimina maji na viungo vyake kwenye kopo kisha liweke
mahali likiwa wazi basi ile harufu huendelea kusambaa chumba kizima

