aina tano za miili

 KUNA MIILI YA AINA TANO 

Ndani ya mwili wetu ipo miili mingine ambayo hufanya kazi kulingana na hali Fulani ya mwili kiujumla miili hii hufanya kazi wakati wa USIKU,hapa nitaelezea kazi za Kila mwili na namna ya kuutambua lakini elewa wenye uweza wa kuutambua ni mwili upi unaotumika huwa Wana ujuzi mkubwa lakini pia wengi hupractise kitu kinachoitwa Astral projection kwa wale wasiojua maana ya astral projection ni kitendo Cha mtu kutoka nje ya mwili wake wakati akiwa amelala na kuutumia katika ulimwengu wa astral, miili hii nitaweza kuilezea Kama ifuatavyo kutokana na experience yangu katika kuitumia

1.physical body

Physical body huu ndio mwili wako halisi au tunaufananisha na hardcopy ni mwili unaooneka na unaweza kushika vitu n.k, mwili huu hutumia milango ya fahamu katika kufanya shughuli zake za kawaida.

2.Dream body/mwili wa ndoto

Mwili huu hauko mbali sana na physical body Mara tu mtu anapoaza kusizia mwili huu huwa tayari kuanza kufanya kazi,japo wakati mwingine si kwamba mtu huwa anatumia mwili huu Bali huwa ni Maono yanayotokana na mawazo yake(hilucination) mwili wa ndoto tunauita kwa jina la soft copy Kila kitu Cha mwili huu hufanana na mwili wa kawaida na Mara nyingi watu hushindwa kutofautisha wanapokuwa wanatumia mwili mf mtu anaweza akawa na uhakika kwamba anakojoa chooni kumbe lo! yupo kitandani,mtu anaweza akahisi anakimbia kumbe lo!amelala kitandani. Unapokuwa unatumia mwili huu Kila kitu huweza kufanana na mwili halisi

3.Energy body

Mwili huu huwa una kazi ya kusambaza energy katika miili mingine unapokuwa kwenye mwili huu hutaweza kujiona mwenyewe hata ukijiangalia kwenye kioo hautaweza kujiona 

Mwili huu huwa hautumiki katika Mambo ya ndoto na mtu atakapoamka kwenye mwili huu hatoweza kukaa sana aidha ataamka au atahamia mwili mwingine

4.etheric body

Huu ni mwili ambao una shape Kama mwili wa kawaida lakini at the same time unaweza kubadilika na kuwa Kama Moshi au upepo hivyo kuutumia mwili huu sio rahisi Mara nyingi watu ambao huongozwa na roho zingine huweza kutumia mwili huu lakini pia zipo incident ambazo humfanya mtu kujikuta anatumia mwili huu

5.Astral body

Huu ndio mwili wenye uwezo mkubwa kuliko yote na ndio upo ndani kabisa baada ya kuipita miili mingine. mwili huu waweza kuchukua shape yeyote hata Kama ni ya mnyama,mwili huu waweza kupita popote hata Kama ni kwenye ukuta,unaweza kusafiri popote kwa mda mfupi hata Kama ni sayari nyingine,mwili huweza kwende kwenye matukio yaliyopita(past), yajayo(future) n.k mwili huu huitaji mtu awe na nguvu kiroho,

Mwili huu ni mgumu zaidi kuufikia Mara nyingi wanaofanya shughuli za kiroho huweza kuutumia huu kwa msaada wa madawa au maombi yanayo husisha roho zingine.

 

 

Post a Comment

Previous Post Next Post