Mambo ya kufanya unapokuwa kwenye mfungo

MAMBO YA KUFANYA UNAPOKUWA KWENYE MFUNGO

Soma neno

Neno la mungu Lina nguvu ya kufanya uponyaji lakini pia unaposoma zaburi huwa pia ni sehemu ya Sala, neno la mungu litakufariji,litakutia moyo na kukupa tumaini katika Yale magumu unayopitia


Fanya maombi

Wakati wa mfungo ni lazima kufanya maombi maana kunakuwa na utulivu katika mlango wa  mawazo na hisia pia hivyo mtu huweza kuomba akiwa na focus ya kutosha

Jihudhurishe mbele za bwana

Unapokuwa kwenye mfungo usipende kufunga mpaka mfungo unaisha haujaenda madhabauni kwa bwana nenda kwenye ibada fanya maombi ukiwa kwenye nyumba ya mungu,

Toa sadaka

Unapokuwa kwenye mfungo toa sadaka zingine kwa mfano sadaka ya shukrani,sadaka za maombi maalumu,sadaka kwa ajili ya Toba n.k hii inakuweka kwenye position nzuri ya kiroho katika kujibiwa maombi yako

 

Acha kuangalia TV,kusikiliza miziki ya kidunia,kucheza magemu na kadhalika

Unapokuwa unafunga hupaswi kufanya Mambo ambayo huwa unayafanya siku zote lazima ustopishe anasa zote za dunia hii na ufanye Mambo yaliyo safi mbele za Mungu

Ondoa chuki,lawama,makwazo na Kila Aina ya fitina ndani ya moyo wako

Chuki,kutokusamehe makosa husababisha mtu kupata maumivu makali ndani ya moyo hivyo kipindi Cha mvungo unatarajia kupata uponyaji wa moyo,hisia zako na mawazo yako kuwa safi

Usiwaelemee watu

Wasaidie watu wenye shida na hata wale wanaokusaidia usiwaelemee Kama Kuna task ambazo wanakufanyiaga Basi Sasa fanya mwenyewe kuwapunguzia mzingo

Pia unaweza kuwapunguzia watu madeni wale unaowadai ambao unajua Wana kipato Cha chini  sana au kuwasamehe kwa wale ambao unajua huyu uwezo wake wa kipato ni mdogo

 

 

 


Post a Comment

Previous Post Next Post